HADITHI; NAKUPENDA MADAM; Sehem ya Tano..........(5)

Tokeo la picha la PICHA ZA WAREMBO

ilipoishia
Mazungumzo yao yaliendelea, wakafika nyumbani kwa mwalimu Magdalena, wakapitiwa na usingizi, kutokana na uchovu waliokuwa nao mwalimu Magdalena na mwalimu Joka wakajikuta wakiamka saa 4 asubuhi, tena baada ya John kuwagongea kutokana na kutomuona mwalimu Magdalena shuleni.



“Sasa itakuwaje, nje kuna hodi inagongwa na sauti ya huyo mtu namjua ni wa shuleni, kama akikuona itakuwa balaa upya, watahisi kuna kitu kimefanyika kati yangu na wewe, sasa naomba ujifiche humu humu ndani mi natoka kumsikiliza.’’



“Sawa.” sasa endelea
Mwalimu Magdalena alipotoka nje akakutana na John, mwanafunzi anayempenda, John hakutaka kuhoji chochote hadi aingie ndani lakini mwalimu Magdalena alionyesha hofu kama ya kusita, lakini akakubaliana na yote, John akaingia akakaa kitandani huku mwalimu Joka akiwa amejificha chini ya uvungu wa kitanda cha mwalimu Magdalena.



“Mwalimu mbona hadi sasa hujafika shuleni kila mtu anahofu nawe, hakuna anayeelewa somo lolote hadi wakuone, mwalimu unanujua wanafunzi wa shule ile tulivyokuzoea na pia kuna taarifa kwamba mwenyekiti alikubaka jana ni kweli mwalimu Magdalena,’’ alihoji John huku uso wake ukionyesha kukasirishwa na kitendo hicho.



“Hapana John hakunibaka, ni kweli lengo lake lilikuwa hilo maana alinikimbiza kichakani usiku mzito lakini alishindwa kufanikiwa.’’



“Alishindwaje wakati mlikuwa wawili? Mi nilijua mwalimu Magdalena huwezi kusubiri unaona sasa, mwenyekiti namchukia maisha yote,’’ alilalama mwanafunzi John huku mwalimu Madgalena akibubujikwa namachozi akishangaa nani katangaza habari hizo akatambua kwamba atakuwa ni mwenyekiti.



“John hapana hakufanikiwa kufanya hicho kitendo ingawa alinikimbiza lakini niliokolewa na mtu mwingine huko msituni alimpiga mwenyekiti akakimbia mimi bado nipo vizuri na nakusubiri John wangu usiwe na hofu,’’ alijibu mwalimu Mgadalena huku wote wawili John na mwalimu Mgdalena wakitokwa na machozi.



Walifutana machozi pale wakajikuta nao wakipitiwa na usingizi. Muda ulipita walipokuja kusituka ilikuwa jioni.



John alistuka kuona muda umekwenda hivyo kwa haraka akaelekea kwao akimwacha mwalimu Magdalena ajiandae kujibu maswali kuhusu John.



Lakini alipoita hakuna aliyeitika na alipochungulia uvunguni hakumuona mwalimu Joka, akashangaa kwa nini hakumuona, alijiuliza maswali mengi asijue alipoelekea mwalimu huyo lakini akili ilimtuma kuamini kwamba mwalimu huyo alitoka wakiwa wamepitiwa na usingizi na John.



Jioni ya saa 12



 Mwalimu Joka alifika kwa mwenyekiti na kujitambulisha kwamba yeye ni mwalimu aliyetakiwa kufika katika kijiji hicho kusaidia kuokoa somo la hisabati lililokuwa likielekea kupotea kwa kuwa hakuna mwanafunzi aliyekuwa akilipenda somo hilo kutokana na kutokuwa na mwalimu wa somo hilo kwa miaka mingi zaidi ya wanafunzi wa kujitolea ambao walifika kijijini hapo kwa mafunzo.



Mwenyekiti alionyesha kutofurahishwa na mwalimu huyo aliyekuwa na umbo la wastani lenye nuru angavu, sura yenye mvuto.



Hofu ya mwenyetiki ni kwamba ujio wa mwalimu huyo ni pigo kwake kumfuatilia mwalimu Magdalena kwa kuwa tayari atapata mlinzi na kwa vyovyote watapendana kwa kuwa wote wametoka mjini, hivyo watakuwa wanapenda maisha yao yaendelee.



Nini kitaendelea hadi kipindi kijacho. Je, mwalimu Magdalena na Mwalimu Joka wakikutana watazungumza nini na je, mwenyekiti atagundua kwamba mgeni wake ndiye aliyemkimbiza porini. Usikose kufuatilia.
Share on Google Plus

About Anonymous

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment