HADITHI; NAKUPENDA MADAM; Sehem ya nne ...............(4)

Tokeo la picha la PICHA ZA WAREMBO
Ilipoishia
Mwalimu Magdalena alikimbia huku akipiga kelele bila kujua anakokimbilia angepata msaada ama la! Alishaanza kuchoka na ilikuwa giza sana, lakini alichoambulia kugundua ni kwamba mtu aliyekuwa akimkimbiza alikuwa amevaa kinyago na nguo nyeusi ili asitambulike. Sasa Endelea
GHAFLA mwalimu Magdalena akajikuta akikamatwa na kufumbwa mdomo, alikukuruka ili ajitoe katika mikono iliyombana vema, lakini hakuweza kuitoa, alijitahidi kujitoa mbele ya mtu huyo aliyemfumba mdomo, sauti pia miguu yake havikumsaidia kufanya chochote kujikwamua kutoka eneo hilo.Mwenyekiti alishangaa kutosikia sauti ya mwalimu Magdalena, akaangaza huku na kule, lakini hakuweza kutambua wapi alipo mwalimu Magdalena, alinyanyua macho huku na huko, lakini hakufanikiwa.

Taratibu Mwalimu Magdalena alikuwa akipoteza nguvu kutokana na kubanwa na asiyemjua, mtu yule alimvuta eneo lingine ili kumkwepa mwenyekiti aliyekuwa akimsaka mwalimu Magdalena ili atimize ahadi yake.

Mwenyekiti alianza kuhamaki alipojificha mwalimu Magdalena, akavua kinyago alichokivaa kuficha uso wake, akaingia katika majani anayohisi mwalimu Magdalena amefichwa.

Mwenyekiti alikanyaga majani yale akiamini mwalimu Magdalena amejificha na yupo peke yake, akazidi kusogea ghafla, naye akashtukia amekabwa na kitu asichokijua.


Mwenyekiti alipiga kelele huku akijitahidi kutoa mkono uliomkaba, lakini hakuweza, akatumia akili za kuruka sarakasi na kujidondosha huku na huko, akapata nafasi ya kujinasua katika mkono huo, hakuwa na ulazima wa kupambana na mtu asiyemjua, akaamua kutimua mbio.

Mwalimu Magdalena taratibu akanyanyuka na kutaka kukimbia, lakini yule mtu aliyemkamata na kumziba mdomo akamkamata kisha akajitambulisha kwake.


“Sitaki, sitaki, sitaki mwenyekiti,’’

“Mwenyekiti, mwenyekiti ndiyo nani mi siyo mwenyekiti, nimekusaidia ulikuwa katika hatari nimekuokoa,’’ walishindwa kuelewana kutokana na giza lililotanda siku hiyo, mwalimu Magdalena alianza kupunguza woga lakini hakutambua sura ya mtu huyo aliyemweleza kuwamba amemuokoa.

Alijitahidi kumtazama lakini hakuweza, mtu huyo alitambua kwamba mwalimu Magdalena anataka kumtambua ni nani, akaingiza mkono wake mfukoni kwake akatoka na simu akawasha tochi kisha akajimulika usoni na kumtaka mwalimu Magdalena amwangalie.

“Wewe ni nani? Umesema ni mwalimu, mwalimu gani na huku umefuata nini?’’ alihoji.

“Mimi ni mwalimu Jokam, wengi wanapenda kuniita Joka.’’

“Joka’’ alihoji kwa hofu mwalimu Magadalena.

“Ndiyo ni Joka kwa kuwa ni mtaalamu wa hisabati, huwa sishindwi chochote katika hisabati na nililetwa kijiji hiki muda mrefu lakini sikupenda lakini kuna jamaa yangu aliniambia aliwahi kufika huku na kuna fursa nyingi huku ndiyo nimekuja kuangalia kama ni kweli nije kufanya kazi huku.’’ Alifafanua mwalimu Joka.

“Tatizo ni nini hadi huyu mwenyekiti akukimbize hivyo.’’

“We acha tu ni story ndefu.’’

“Nisimulie nitakusaidia.’’

“Najua utanisaidia, ila turudi kwanza nyumbani kisha kesho asubuhi nitakuhadithia kama unataka.’’

“Sawa ila mimi ni mwenyeji wa mwenyekiti.’’

“Sasa mwenyekiti mwenyewe ndiyo huyo umemtimua.’’

“Kazi ipo kweli kweli sasa nifanyeje?’’

“Twende kwangu mambo mengine yote utajua asubuhi, maana ni usiku na umenisaidia sana kuniokoa, ila mimi sihitaji hata fursa zilizopo, kesho mapema nitaanza safari ya kurudi mkoani kwetu bora nikawe mama wa nyumbani huko kuliko kuteseka hapa na mwenyekiti,’’ alilalama mwalimu Magdalena.

“Ahaaa! Huyu mwenyekiti ndiyo akusumbue wewe nitadeal naye we niachie mimi tena nitamweka wazi kwa watu wote, kwani hana mke.’’

“Hata sijui,’’ alijibu mwalimu Magdalena.

Mazungumzo yao yaliendelea, wakafika nyumbani kwa mwalimu Magdalena, wakapitiwa na usingizi, kutokana na uchovu waliokuwa nao mwalimu Magdalena na mwalimu Joka wakajikuta wakiamka saa 4 asubuhi, tena baada ya John kuwagongea kutokana na kutomuona mwalimu Magdalena shuleni.

“Sasa itakuwaje, nje kuna hodi inagongwa na sauti ya huyo mtu namjua ni wa shuleni, kama akikuona itakuwa balaa upya, watahisi kuna kitu kimefanyika kati yangu na wewe, sasa naomba ujifiche humu humu ndani mi natoka kumsikiliza.’’

“Sawa.” 
Unadhani nini kitaendelea hapo ikitokea John akibaini kuwa mwalimu magdalena yuko ndani. usiko kipindi kijacho..... 
Share on Google Plus

About Anonymous

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 Comments:

Post a Comment