FREEDOMLEO BLOG
Ugonjwa wa ukimwi ni ukosefu wa
kinga mwilini baada ya virusi aina ya lentivirus kushambulia chembe chembe nyeupe za damu zenye uwezo wa kuukinga mwili
usishambuliwe na magonjwa mbalimbali.
Ugonjwa huu umegundulika katika
karne 19 na 20 baada ya virusi aina ya simian immunodeficiency virus (Siv)kutoka
kwa wanyama aina ya Sokwe na kwenda kwa binadamu na kubadilika kuwa human
immunodeficiency virus(HIV) huko jangwa
la Sahara huku ukigawanyika katika makundi makuu mawili HIV-1 NA HIV2.
HIV-1 iligundulika kusini mwa Cameroon
kutoka kwa sokwe hadi kwa binadamu na HIV2 imetokana na nyani waliofahamika kwa jina la Sooty
Mangabey ambao walikuwa wanapatikana Afrika
Magharibi na kusini mwa Senegal.
Zipo nadharia mbalimbali zinazoelezea chanzo,
chimbuko na asili ya ugonjwa huu wa ukimwi nazo ni,
1:NADHARIA YA UWINDAJI.
Nadhari hii inaelezea kuwa ugonjwa wa ukimwi umetokana na virusi aina ya simian immenodiffiency virus(SIV) kuhamia kwa binadamu baada ya kula nyama mbichi ya sokwe waliowaua au damu kuingia kwenye vidonda vya wawindaji hao ilionekana bara la Afrika kati ya miaka 1980.
Nadhari hii inaelezea kuwa ugonjwa wa ukimwi umetokana na virusi aina ya simian immenodiffiency virus(SIV) kuhamia kwa binadamu baada ya kula nyama mbichi ya sokwe waliowaua au damu kuingia kwenye vidonda vya wawindaji hao ilionekana bara la Afrika kati ya miaka 1980.
2:NADHARIA YA KINGA YA
POLIO.
Inaelezea chimbuko la ukimwi
kuwa ulianza kwenye majaribio ya chanjo ya polio iliyojulika kwa jina la CHAT
iliyotolewa kwa watu takribani milioni moja wa CONGO,RUANDA na BURUNDI kati ya
miaka 1950 huku ikisemekana ya kuwa chanjo hiyo ilikuzwa ndani ya seli za figo
za sokwe walikuwa na virusi aina ya simian immenodifficieny virus na kusababisha watu kupata HIV-1.
3:NADHARIA YA SINDANO.
Nadharia hii ni muendelezo wa
nadharia ya uwindaji inasema ya kwamba katika miaka ya mwanzo ya 1950 sindano
zilianza kutumika ingawa ilikuwa ni kwa mara chache sana katika nchi za Afrika
huku wafanyakazi wa idara ya afya waliendelea kutumia sindano moja kwa watu
wengi kutokana na hili suala inawezekana kuwa ilieneza virusi kutoka kwa mtu
mmoja kwenda kwa mwingine.
4:NADHARIA YA UKOLONI.
Katika miaka ya mwanzo ya karne
ya 19 na ya mwisho ya karne ya 20 ukoloni uliingia katika maeneo mbalimbali Afrika
ikiwemo maeneo ya BELGIAN CONGO na
FRENCH EQUATORIAL AFRIKA ambapo watawala hawakuwathamini watu walio watawala
kutokana na hali hii wa Afrika wengi walijikuta wakiwa kwenye makambi ambako
hali ya usafi zilikuwa duni na chakula kilikuwa kichache kutokana na hali hiyo
ili wapasa kula nyama za sokwe kutokana na afya zao kuwa duni virusi waliwashambulia
kwa urahisi na kudungwa sindano zisizochemshwa.
5:NADHARIA YA UANGAMIZAJI.
Nadharia hii inaelezea ya kwamba ukimwi ulitengenezwa nchini MAREKANI na shirika la US-FEDERAL SPECIAL CANCER VIRUS PROGRAM ikiwa ni njama ya kuua watu weusi na watu wanao shiriki mapenzi ya jinsia moja (mashoga) kote duniani.
Nadharia hii inaelezea ya kwamba ukimwi ulitengenezwa nchini MAREKANI na shirika la US-FEDERAL SPECIAL CANCER VIRUS PROGRAM ikiwa ni njama ya kuua watu weusi na watu wanao shiriki mapenzi ya jinsia moja (mashoga) kote duniani.
0 Comments:
Post a Comment